ZIFAHAMU AINA KUMI (10) ZA SUNGURA

1.       New Zealand Whites: Hii ni jamii mojawapo maarufu kwa ufugaji wa sungura wa nyama, na kwa nchi kama Marekani, nyama yake ndiyo bora zaidi kuliko aina nyingine za sungura. Sungura hawa wanaweza kufikisha kilogramu 3.6 hadi 5.
2.       Californian Rabbits: Hawa ni uzao chotara wa sungura jamii ya Chinchilla na New Zealand Whites. Wana manyoya meupe na madoa meusi na wanafahamika kutokana na maumbile yao kama matofali na wanatoa nyama nzuri. Wanaweza kufikisha kilogramu kati ya 3.2 hadi 4.8.
3.      American Chinchilla : Hawa ni aina bora ya sungura kwa ajili ya nyama na wanarandana na sungura jamii ya Chinchilla ambao hata hivyo ni wakubwa kwa maumbo. Wana rangi ya kijivu na nyama yao inaweza kufikisha hadi kilogramu 3.6. Nyama yake inapendelewa Zaidi kukaangwa ama kubanikwa.
4.      Silver Foxes: Hawa ni sungura rafiki zaidi kufugwa majumbani ambao wanafaa kwa mapambo pamoja na nyama. Aina hii ni adimu sana na wanaweza kufikisha kilogramu kati ya 4 hadi 5. Wana rangi ya fedha yenye kivuli cheusi na masikio yeliyoinuka, kama alivyo mbweha wa rangi ya fedha.
5.       Champagne D Argent: Aina hii ya sungura wa kihistoria anayevutia imetumiwa kwa nyama tangu mwaka 1631. Nyama yao inapendwa ulimwenguni kote na ni wazuri kwa kufugwa. Unaweza kuwakuta katika rangi mbalimbali kama nyeupe, rangi ya maziwa au chocolate.
6.       Cinnamons: Hawa ni uzao chotara kati ya sungura wa New Zealand White na American Chinchilla. Maumbile yao yamerandana na asili yao. Sungura hawa wanatoa nyama nzuri na wanafugwa zaidi kibiashara kwa ajili ya nyama.
7.      Satins: Hawa ni sungura wakubwa na wazito ambao wanatoa kiwango kikubwa cha nyama. Ni wazuri kwa kufugwa kwa ajili ya nyama. Maumbile yao ni ya kati na wanapatikana katika rangi mbalimbali kama bluu, nyeusi, shaba, chocolate, nyekundu, Siame na otta.
8.       Rex: Sungura hawa wenye manyoya laini yanayoteleza hufugwa kwa ajili ya manyoya na nyama. Wanapokuwa wakubwa wanaweza kufikisha kati ya kilogramu 3.2 hadi 4. Wana rangi za bluu, amber na madoa meupe. Nyama yao ni nzuri na wanafaa sana kufugwa.
9.      Palomino: Hawa ni jamii bora ya nyama na wanafugwa kibiashara kwa ajili ya nyama tu. Ni wapole na wanafaa kufugwa nyumbani. Wanaweza kufikisha kati ya kilogramu 3.2 hadi 4.5.
10.  Flemish Giants: hawa ni sungura wakubwa na mabanda yao lazima yajengwe kwa ukubwa wa mita moja urefu.Ukubwa kamili hufikiwa bada ya miezi 9. Hawazaliani kwa haraka lakini wanaweza fikisha watoto 12 kwa mzao mmoja. Sungura aina ya 01,02,03 na 09 tayari wanapatikana Tanzania katika mikoa ya Arusha, DSM na Kilimanjaro

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Udongo

KAZI YA KILIMO TANZANIA.

Watu wengi kwenye vyombo vya habari wanalalamika maranyingi wakiwemo vijana, wazee na watu wa umri wa kati kuwa hakuna kazi. Je, hivi nikweli kuwa hakuna

Read More »

Kilimo Cha Maharage Ya Njano.

Kilimo cha maharage ni rahisi na kinalipa sana kikifanyika kwa utaalamu. Gharama nafuu na ushindani wa soko sio mkubwa sana. Huhitaji kusafiri, kinachofanyika ni kuwaita

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »