UGONJWA WA COLIBACILLOSIS KWA KUKU: Ugonjwa huu husababishwa na bakteria waitwao Escherichia coli. Bakteria hawa huingia mwilini kwa mnyama kwa njia ya chakula au mara tu mnyama anapozaliwa au kuku anapototolewa.
– Bakteria hawa huanza mashambulizi mara tu mnyama anapopata matatizo (stress) kwa vile kinga ya mwili hupungua.
WANYAMA HUSIKA:
• Ugonjwa hujitokeza hasa kwa vifaranga( kuanzia wiki 2-4), ndama, watoto wa mbuzi, kondoo, farasi mara tu baada ya kuzaliwa (Neonatal diarrhoea).
• Wanyama wakubwa huwa kama wabebaji wa vijidudu (Carriers) na kinyesi chao mara nyingi ndiyo chanzo cha ugonjwa huu.
DALILI KWA VIFARANGA:
• Kutokuwa na raha (depression)
• Kuacha kula
• Kuharisha uharisho mweupe
• Rangi ya kilemba na mashavu kupauka
• Vifo
VIFARANGA VIKIFA HUONYESHA DALILI ZIFUATAZO:
• Ini na bandama huvimba na huwa na vidoadoa vya damu (haemorrhage)
• Ukungu wa usaha kwenye ini, na vifuko vya hewa (Air sacs) kwenye mapafu
• Uchafu wa majimaji nje ya viungo vya mwilini.
DALILI KWA NDAMA, WATOTO WA MBUZI, KONDOO N.K
– Ugonjwa mkali (Acute form)
• Kuharisha mfululizo
• Kupungua maji mwilini
• Kufa ndani ya masaa 12
– Ugonjwa wa makali ya (wastani) kati (Subacute form)
• Kuharisha kwa muda mrefu – Siku kadhaa
• Kupungukiwa maji mwilini
• Kukonda
• Kufa kama tiba haikupatikana haraka
• Mnyama akifa utumbo (ndani) huwa umejaa makamasi (mucoid enteritis)
TIBA
KUREKEBISHA HALI YA MWILINI
(i) Upunguaji wa maji, madini na vitamini hurekebishwa kwa kutumia dawa za kufunga kuharisha Kaovit R na vitamini
kama vile vitalyt, Vitastress na dawa zingine kama Sodium, Glucose
(ii) Wape wanyama wagonjwa chakula kizuri chenye protini ya kutosha
DAWA ZA KUTIBU
- Doxycol katika maji ya kunywa
KINGA
1. Colirid – Kinga katika chakula: Dawa hii huzuia colibacillosis kwa kuua wadudu ndani ya mwili wa kuku/mnyama
2. Farmacid premix – Dawa hii huchanganywa na chakula na huzuia collibacillosis kwa kuua na kuzuia vijidudu (E.coli) katika chakula kabla ya kuliwa na kuku au mnyama husika.
– Ndama, watoto wa mbuzi n.k- Wapate maziwa ya mwanzo ya mama (colostrum) mara baada ya kuzaliwa, kama mama amekufa mtoto apatiwe ‘artificial colostrum’
– Vifaranga wapewe antibacterials ndani ya wiki moja baada ya kutotolewa.
– Usafi wa mazingira, vyombo na wahudumu.
– Wanyama wakubwa wasichanganywe na wadogo (newborns)