HIZI NDIZO MBINU ZA KUZUIA WADUDU, NDEGE NA WANYAMA WAHARIBIFU WA MAZAO

Wadudu

Wadudu wanaoweza kushambulia mazao ni pamoja na katapila na jongoo

.Katapila

  • Hukata ncha ya mmea inayokua

Kudhibiti

  • Kagua shamba mara kwa mara ili kutambua kuwepo kwa wadudu hao na kuwaua.

Jongoo

Jongoo
  • Hukwangua shina na kuacha michubuko

Kudhibiti

  •  Kagua shamba mara kwa mara na kuwaua.

Kuku

  • Huharibu mmea kwa kuparura juu ya ardhi na kusababisha kujeruhi na kukata mizizi. Uharibifu huu husababisha mmea kuwa katika mazingira rahisi ya kushambuliwa na vimelea kama Fusarium batatis ambao huozesha mizizi ya mmea.

Kudhibiti

  • Zuia kuku wasiingie shambani.

Konokono

  • Husababisha uharibifu zaidi kipindi cha mvua. Wanapotambaa kwenye mmea huacha utando, hasa katika sehemu inayochipua na kusababisha mmea kudumaa.

Kudhibiti

  • Kagua shamba mara kwa mara na kuwaondoa.
  • Weka mchanganyiko wa mbolea ya samadi na majivu kuzunguka shina la mmea ili kuzuia wasiweze kupanda juu ya mimea.

ANGALIZO: Ni muhimu kupulizia / kunyunyizia dawa uharibifu ukiwa mkubwa sana. Tembelea maduka ya Kilimo kwa aJili ya Ushauri Zaidi na kununua Dawa.

PITIA
Kilimo cha bamia sehemu ya pili (02)

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Udongo

KAZI YA KILIMO TANZANIA.

Watu wengi kwenye vyombo vya habari wanalalamika maranyingi wakiwemo vijana, wazee na watu wa umri wa kati kuwa hakuna kazi. Je, hivi nikweli kuwa hakuna

Read More »

KILIMO BORA CHA TANGAWIZI

UTANGULIZI Tangawizi ni aina ya zao la kiungo ambalo sehemu inayotumika ni tunguu ( rhizome) ambalo huonekana kama mizizi ya mmea. Kwa jina la kitalamu ni Zingiber

Read More »

FAIDA ZA MBOLEA YA MBOJI

Matumizi ya mbolea ya mboji katika kilimo cha mazao yana faida zifuatazo; Utengenezaji wa mbolea ya mboji hauna gharama na ni rahisi hivyo wakulima wa ngazi

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »