JINSI YA KUJITENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWA AJILI YA KUONGEZA UZALISHAJI

Kutokana na kuongezeka kwa gharama za chakula cha kuku iwewawia vigumu wafugaji wa kuku kupata faida kupitia ufugaji wa kuku. N akwa jinsi utengenezaji wa chakula cha kuku hasa hasa kuku wa kisasa kama broiler na layers kwa wafugaji ni ngumu leo nakuja na somo jepesi la jinsi ya kutengeneza chakula kwa kuku chotara (hybrid) or kuku wa kienyeji wanaofugwa ndani ya banda kwa kutumia Pearson Square method nah ii yote yawezekana kama mkulima atakuwa na raw materials zinazohitajika katika utengenezaji wa chakula.

Njia HII ya pearson square mara nyingi ina base sana katika Digestable crude protein (DCP) ya malighafi husika katika utengenezaji wa chakula. Na malighafi zinazotahitajika hapa ni kama vile Mahindi, mashudu ya pamba, mashudu ya alzeti, maharage ya soya na dagaa.

Jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku wa mayai (70kg) (chotara) unahitaji vifuatavyo;

34 kg Mahindi

12 kg Soya beans

8 kg Dagaa

10 kg pumba za mahindi

6 kg Chokaa (kwa ajili ya calcium)

Jinsi ya kutengeneza chakula(70kg) kwa ajili ya kuku wa nyama

Mahindi= 40 kg

Dagaa = 12 kg

Maharage ya soya = 14 kg

Chokaa = 4 kg

NB: Hakikisha unaongeza chumvi 250g katika kila mfuko wa 70kg wa chakula chako

Ndondoo muhimu ya jinsi ya kuwalisha kuku wako Nyumbani

· Kuku anaetaga mayai anahitaji kula angalau 130g za chakula kwa siku. Kumbuka kuwapa maji masafi muda wote.

· Kifaranga kimoja anahitaji 2.2 kg za chakula kwa wiki 8 (hivyo basi vifaranga 100 = 2.2 kg x 100=220 kg. Vifaranga wanahitaji kula muda wote na pia suala la maji ni muhimu kwao pia na unakumbushwa kuwapa mboga mboga baada ya mlo wao kuisha.

PITIA
Vyakula Vinavyoongeza Hamu Ya Tendo La Ndoa Kwa Haraka Kwa Mwanamke

Kuku mdogo anayekaribia kutaga anatakiwa kula 4.5 kg ya chakula kwa muda wa miezi miwili na nusu mpaka watakapoanza kutaga yai kwa mara ya kwanza. Baada ya hapo wanabadilishiwa chakula na kupewa chakula cha utagaji (layer diet).

· Malighafi zinazotakiwa katika utengenezaji wa chakula zinatakiwa zile za kiwango cha juu kabisa usitumie mahindi yenye uozo maana utafanya kuku wako kupata ugonjwa wa aflatoxins poisoning.

Ukitumia dagaa hakikisha ni wasafi na hawana mchanga ama shells wa aina yoyote.

· Na mwisho hakikisha chakula hicho unakichanganya vizuri kabisa ili kuleta uwiano au mchanganyo ulio sahihi.

Hitimisho

Kwa formular za Chakula za Kuku wa kisasa kama Broiler na Layer tunaweza wasiliana kwa namba zangu hapo chini na hakika zitakuongezea uzalishaji maradufu ya chakula cha kununua.

Imeandaliwa na Dr of Veterinary Medicine

Phone: 0712784472

theriogenology

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Kilimo cha Mpunga Tanzania

MPUNGAHili ni zao la chakula linalolimwa kwa wingi kwenye maeneo ya ukanda wa joto. Zao hili linastawi zaidi kwenye udongo wa tifu tifu na eneo

Read More »

SABABU ZINAZOWEZA KUATHIRI CHANJO

SABABU ZINAZOWEZA KUATHIRI CHANJO SABABU ZINAZOWEZA KUATHIRI CHANJO KUTOA KINGA KWA KUKU INGAWA WAMECHANJWA : Uzoefu umeonyesha kuwa wafugaji wengi wa kuku wa kisasa(Commercial Chicken)

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »