JINSI YA KULEA VIFARANGA VYA KUKU SEHEMU YA KWANZA(1)

Karibu mpenzi msomaji wa KILIMO TANZANIA , leo hii napenda kuwaletea soma la jinsi ya kulea vifaranga vya kuku, hivyo tusiache kua nasi ili kujifunza mengi zaidi.
Na tutaanza na jinsi ya kujenga nyumba ya vifaranga, hivyo ukitaka kujenga nyumba ya vifaranga nilazima uzingatie yafuatayo.
  • Nyumba ya vifaranga nilazima ijengwe karibu na nyumba ya muangalizi hii ni kwaajiri ya kuweza kuwa karibu kwa uangalizi zaidi.
  • Nyumba ijengwe hatua 20 au zaidi mbali na nyumba ya kuku wakubwa hii nikwaajili ya kupunguza maambukizi ya magonjwa.
  • Nyumba ya vifaranga isiruhusu unyevu, baridi na wanyama au wadudu kuingia ndani, lakini ni lazima iwe na mwanga wakutosha
  • Pia nyumba ya vifaranga inatakiwa kua na uwazi wa kutosha kuwezesha vifaranga kutobanana na waweze kutembea kwa uhuru.
  • pia ijengwe eneo ambalo haliruhusu upepo kutoka kwenye nyumba ya kuku wakubwa kuingia hii itapunguza maambukizi ya magonjwa.
 UKUBWA WA NYUMBA
Ukubwa, vifaranga hawaitaji eneo kubwa katika wiki 4 za mwanzo, kwa makidirio mazuri mita squire moja huchukua vifaranga 16, na baada ya wiki 4 za mwanzo unatakiwa kuongeza eneo ili kuwapa nafasi zaidi.
Sakafu, sakafu inayo faa ni ile ya simenti ikichanganywa na zege au unaweza kuchukua kinyesi cha ng’ombe kilicho changanywa na maji kisha ukasiliba chini, unaweza kuchagua aina gani ya sakafu kati ya hizo kulingana na uwezo wako.
Ukuta, unaweza kujenga ukuta kwa kutumia matofari, bati, mabanzi au debe kulingana na uwezo wako, urefu unatakiwa kua futi 6-8 kutoka chini kwenda juu futi 3-4 za chini nilazima zizibwe na ukuta na futi 3-4 za juu unaweka wavu wa chuma au fito kulingana na uwezo wako, na ukuta ulio jengwa kwa tofari nilazima upigwe lipu.
Dirisha, madirisha yanaweza kuzibwa kwa kutumia mabokis au mkeka ikishwa wekwa nyavu, kulingana na uwezo wako.
Paa, Paa nilazima liwe zuri lisilo vuja na unaweza kuweka tundu la kutoa hewa y joto
Nitumaini langu umepata elimu ya kutosha na usisite kua nasi ili kuendelea kupata elimu zaidi.
PITIA
UFUGAJI WA BATA KAMA FURSA YA KIPATO

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

MFAHAMU KUKU AINA YA KUCHI

Ni kuku warefu kwa umbo na wenye kusimama mgongo ukiwa wima. Wana manyoya machache mwilinini na hasa kifuani, vilemba vyao ni vidogo. Majogoo huwa na

Read More »

Kilimo bora cha nyanya -Tz

Utangulizi Nyanya ni zao la mboga linalolimwa sehemu nyingi duniani kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na pia kama zao la biashara. Nyanya ni aina

Read More »

Afisa Kilimo

Afisa kilimo Mkoa wa Mbeya  akipokea maelezo ya kilimo cha mboga ndani ya hema maalumu ya kuoteshea nyanya iliyowekwa na Barton Tanzania kwa ushirikiano na

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »