KILIMO BORA CHA VIAZI MVIRINGO

UTANGULIZI

Viazi mviringo ni zao muhimu la chakula na biashara katika nchi nyingi zinazoendelea. viazi husitawi vizuri sehemu zenye miinuko kati ya mita 1300 hadi 2700 juu ya usawa wa bahari. hukomaa katika kipindi cha miezi mitatu hadi mitano.

viazi mviringo vina virutubisho  vingi mfano vitamin, protin,madini na maji

           SIFA ZA MBEGU BORA ZA VIAZI

 

  • Zenye kutoa mazao mengi zaidi kutoka kwenye shina moja
  • ziwe zimechipua vizuri na ziwe na machipukizi mengi zaidi ya manne
  • zisiwe na wadudu pamoja na magonjwa
  • zitoke katika aina ambayo haishambuliwi na magonjwa kama vile ukungu na mnyauko
  • zenye ukubwa wa wastani unaolingana na ukubwa wa yai la kuku
  

mfano wa viazi mviringo

AINA BORA YA VIAZI MVIRINGO

Kuna aina nyingi sana ya viazi mviringo lakini hapa nitataja aina ambazo nazifahamu na ni bora

kutoka taasisi ya utafiti wa kilimo uyole

  • baraka
  • sasamua
  • tana
  • subira(EAI 2329)
  • Bulongwa
  • kikondo(CIP 720050)

MUDA WA KUPANDA

Viazi mviringo mara nyingi katika maeneo mengi vinapandwa agost hadi september na november hadi december

 

Natumia sentimita 60 hadi 75 kutoka mstari hadi mstari na nafasi kati ya kiazi na kiazi ni sentimita 30.

   MBOLEA

Ili kupata mazao mengi kutoka shambani mkulima anashauriwa kutumia mbolea aina ya samadi, mboji, maan mabichi  na za viwandani

kwa mbolea za viwandani tumia kilo 300 au mifuko 6 za mbolea ya TSP kwa hekta moja, ns kilo 300 mifuko 6 za mbolea ya CAN au kilo 400 mifuko 8 ya SA au kilo 175 mifuko 3.5 za UREA.

  PALIZI

Palilia viazi wiki mbili au tatu baada ya kuchomoza. inulia udongo kufanya tuta zuri ili pawepo na unyevu wa kutosha na kufunika viazi kutokana na mwanga wa jua

PITIA
FAIDA ZA UFUGAJI NYUKI

MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU

Ili kuzuia ugonjwa wa ukungu tumia Ridomil.

changanya gram 100 za dawa  katika lita 20 za maji na nyunyuzia mara baada kila wiki mbili au tatu kutegemea na hali ya hewa.

nyunyuzia dawa ya karate kiasi cha mililita 20 mpaka 40 za dawa katika lita 20 za maji ili kuzuia wadudu kama inzi weupe na wengine. Tumia mbinu bora za kilimo kama usafi wa shamba au kilimo mzunguko kama mbinu ya kuzuia magonjwa na wadudu.

KUVUNA NA MAVUNO

Viazi huwa tayari kuvunwa baada ya miezi 3 hadi 5 kutoka kupanda. mda wa kuvuna unategemea na mda wa kupanda na dhumuni la zao

usiache viazi shamban bila kufunika  kwa nyasi au udongo  kwa mda mrefu

KUHIFADHI

Viazi vya chakula viiafadhiwe kwenye ghara hewa ya kutosha pasiwe na unyevunyevu na joto kali

 
                                         mfano wa chakula kinachotokana na viazi mviringo

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »