MIVARF yaboresha soko la Vitunguu swaumu

Sehemu ya Ghala la kuhifadhi vitunguu Saumu liliojengwa na MIVARF, lipo Mkoani Manyara Wilayani Mbulu, kijijini Bashay. Ghala hilo lina uwezo wa kuhifadhi tani 50 za vitunguu Saumu.
Na. Ibrahim Hamidu
Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) imeboresha Soko la Vitunguu Saumu kwa kujenga ghala la kuhifadhi vitunguu mkoani Manyara, wilayani Mbulu katika kijiji cha Bashay.
Ghala hilo lenye uwezo wa kuhifadhi tani 50 za vitunguu, limegharimu Jumla ya shilingi milioni 88 ikiwa MIVARF imechangia asilimia 95 ya fedha hizo na Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imechangia asilimia 5 ya fedha hizo.
Akiongea na timu ya wataalam kutoka MIVARF ofisini kwake hivi karibuni wakati timu hiyo ilipokuwa ikikagua utekelezaji wa shughuli za Mradi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Bw. Nicholaus Haraba, alifafanua kuwa ujenzi wa ghala hilo umeongeza mnyororo wa thamani wa zao la vitunguu Wilayani Mbulu.

PITIA
Kilimo Bora Cha Alizeti

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Njoo ujifunze kilimo cha nyanya

NYANYA ni zao linalopendwa kutumiwa….kunogesha chakula, chakula kilichowekwa NYANYA huwa na radha nzuri inayomvutia mlaji Wakulima wengi hutamani kulima zao hili wengi huandika FAIDA na

Read More »

Kilimo bora cha Ndizi

Hapa Tanzania kilimo cha migomba kimekuwepo Kwa miaka mingi. Kilimo hiki ni maarufu sana kwa sababu zao la ndizi limekuwa likitumika kama chakula kikuu kwa

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »