MYCOTOXINS NI MOJA YA CHANGAMOTO KATIKA UZALISHAJI KUKU

MADHARA YA MYCOTOXINS KWA KUKU
MADHARA YA MYCOTOXINS KWA KUKU

MYCOTOXINS NI MOJA YA CHANGAMOTO KATIKA UZALISHAJI KUKU : Mycotoxins ni kemikali sumu zinazotolewa na fangasi (molds) na huathiri wanyama na binadamu. Sumu hizi pia hushika na kujiambukiza katika nafaka ambazo bado zipo shambani,wakati wa kuvuna, kusafirisha au kuhifadhi kwenye ghala katika hali ya unyevunyevu na wakati hali ya hewa inapobadilika.

Mycotoxins maarufu zinazoathiri ufugaji wa kuku ni kama ifuatavyo:

Aflotoxins – hutolewa na Aspergillus flavus, Aspergillus parasiticas

Ochratoxins – hutolewa na Aspergillus ochraceus

Trichothecenes – hutolewa na Fusarium spp.

Zearalenone – hutolewa na Fusarium spp

Fumonisins – hutolewa na Fusarium spp.

Inakisiwa kuwa asilimia 25% ya mazao ya dunia huambukizwa mycotoxins na huleta hasara kubwa katika ufugaji wa kuku wa biashara.

MADHARA YA MYCOTOXINS KWENYE MAHINDI
MADHARA YA MYCOTOXINS KWENYE MAHINDI

Mycotoxins huathiri kuku kwa njia nne kubwa:

• Hupunguza hamu ya kula

• Hupunguza kufyonzwa kwa virutubisho vya chakula mwilini

• Huathiri mfumo mzima wa homoni za mwili

• Hupunguza kinga za mwili za kupambana na magonjwa. Na hili ndilo tatizo kubwa katika ufugaji kuku; kwa sababu huwafanya kuwa dhaifu katika kukabiliana na magonjwa mbalimbali.

Pia mycotoxins hupunguza uwezo wa dawa za kutibu na kufanya kazi yake (Lower drug efficiency) na hupunguza uwezo wa chanjo kufanya kazi yake (Lower vaccine response)

MYCOTOXINS NI MOJA YA CHANGAMOTO KATIKA UZALISHAJI KUKU
MYCOTOXINS NI MOJA YA CHANGAMOTO KATIKA UZALISHAJI KUKU

Tatizo la mycotoxins pia ni changamoto kubwa kwa wazalishaji wa mazao ya mimea

KINGA

Ni vigumu kukinga maambukizo ya mazao kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, hata hivyo kutambua nafaka zilizoambukizwa ni jambo muhimu katika kupambana na sumu hizo.

• Kuangalia hali ya nafaka kwa macho na pia kupima katika maabara

• Kujitahidi kupunguza nafaka zisivunjike kwa wingi wakati wa kubangua

PITIA
KILIMO BORA CHA VIAZI MVIRINGO

• Kuhifadhi nafaka vizuri, kuzuia unyevu, joto kali, wadudu waharibifu kama vile panya.

• Kwa nafaka zilizoanza kuathirika au kwa kukinga athari hizo njia pekee bora ni kutumia vifyonza sumu (mycotoxins adsorbent) kama vile MYCOBIND.

• Kuchanganya vitu ambavyo vinapambana na fangasi zinazotoa sumu kama aspergillus na fusarium kwa kuongeza kiasi cha tindikali katika vyakula na mifugo. Dawa za kuongeza tindikali katika vyakula ni kama vile FARMACID PREMIX.

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Kilimo cha Tangawizi

Kilimo cha tangawizi kimekuwa kikiwapa unafuu wakulima wa sehemu nyingi hapa nchini hasa katika mkoa wa Kilimanjaro katika wilaya ya same Tukisema kuna mikoa iliyo

Read More »

AINA ZA UDONGO ZINAZOPATIKANA TANZANIA

Udongo ni rasilimali muhimu inayotumiwa katika shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo ambacho kinategemewa na watanzania kuendesha uchumi wa taifa. Lakini uharibifu wa mazingira umechangia kushuka kwa

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »