UCHANGANYAJI WA VYAKULA VYA MIFUGO

Kwanza ifahamike kuwa kuna formular nyingi Sana unazoweza kuzitumia kwa lengo la kutengeneza chakula cha mifugo yako lengo tu ni uweze kupunguza angalau gharama za uendeshaji wa mradi wako, Hapa mimi nawapa mojawapo ya formular hizo na faida ya kujua kuchanganya chakula peke yako nyumbani ni kupunguza gharama za kununua chakula cha kiwandani, uweze kutumia malighafi zinazopatikana eneo lako nk.
Ili kuweza kufikia huko unahitaji vitu ama malighafi utakazozitumia ili ziweze kukupatia virutubisho vikuu anavyohitaji mfugo wako ili aweze kukuzalihishia unachokitaka na virutubisho hivyo ni proteins, vitamins, madini, fat, na carbohydrates.
Malighafi tutakazotumia hapa ni pumba mahindi =carbohydrates, Mashudu alizeti=protein+fat, dagaa sagwa=protein+madini, chokaa mifugo=madini, and madini mchanganyiko/premix=madini na chumvi=madini.
CHAKULA CHETU TUTAKACHOTENGENEZA NI CHA KILO 100.
VIFARANGA NYAMA ANZA /BROILER STARTER
Pumba mahindi…. 76kg
Mashudu alizeti…. 12kg

Dagaa sagwa…….. 10kg

Premix… ……………..0.5kg

Chokaa mifugo….. 1kg Chumvi sagwa……0.5kg

VIFARANGA NYAMA KUZIA
Pumba mahindi 76kg
Mashudu alizeti 15kg

Dagaa sagwa 7kg

Premix 0.5kg

Chokaa mifugo 1kg

Chumvi sagwa 0.5kg

Pumba mahindi 76kg
Mashudu alizeti 16kg

Dagaa sagwa 5kg

Premix 0.5kg

Chokaa mifugo 2kg

KUKU MAYAI KUZIA

Chumvi sagwa 0.5kg

Pumba mahindi 80kg

Mashudu 12kg

Chokaa 2kg

Dagaa 5kg Premix 0.5kg

KUKU MAYAI TAGA

Chumvi 0.5kg

Pumba 80kg
Mashudu 14 kg

Dagaa 3kg

Premix 0.5kg

Chokaa 2kg

NGURUWE WATOTO

Chumvi 0.5kg

Pumba 76kg
Mashudu 15 kg

Dagaa 6kg

Premix 0.5kg

Chokaa 2kg

NGURUWE KUKUZIA

Chumvi 0.5kg

Pumba 78kg
Mashudu 15kg

Dagaa 4kg

Premix 0.5kg

Chokaa 2kg

NGURUWE NENEPESHA

Chumvi 0.5kg

Pumba 80kg
Mashudu 15kg

Dagaa 2kg

Premix 0.5kg

Chokaa 2kg

NG’OMBE MAZIWA

Chumvi 0.5kg

Pumba 80kg
Mashudu 17kg

Chokaa 2kg

Chumvi 0.5kg

Premix 0.5kg

NOTE PALIPOANDIKWA PREMIX, HIZI HUWA ZINAUZWA MADUKA YA MIFUGO SASA UTAKACHOFANYA KAMA KUKU WAKO NI WA MAYAI NA WAPO KWENYE UMRI WA GROWER UTANUNUA GROWER PREMIX, KAMA WANATAGA UTANUNUA LAYER PREMIX, HIVYO HIVYO KAMA NI WA NYAMA UTANUNUA BROILER PREMIX, KAMA NI NG’OMBE UTANUNUA CATTLE PREMIX, NA KAMA NI NGURUWE UTANUNUA PIG PREMIX
Pia sehemu yenye Pumba mahindi unaweza usiweke tu pumba yenyewe bali unaweza kuchanganya pumba nusu na paraza nusu kwa mfano kama pumba imeandikwa 76kg unaweza kugawa nusu 38kg ikawa pumba na hiyo 38kg nyingine ikawa paraza lakini iwe tu ni kwa kuku isiwe kwa nguruwe au ng’ombe, na pia sehemu yenye chokaa unaweza ukagawa ikawa chokaa na mifupa sagwa ukifanya hivi chakula chako kitakua vizuri zaidi.
KUKU KIENYEJI/BATA
UJAZO NI KILO 50.
Pumba mahindi 38kg

Mashudu 7kg

Mifupa/chokaa 2kg

Dagaa 2kg

Chumvi 0.5kg

Premix 0.5kg

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Kilimo cha Tufaa

Tufaa ni tunda moja maarufu duniani ambalo hupendwa kuliwa na watu wa jamii zote, hii inatokana na utamu wake pamoja na faida za kiafya zinazopatikana

Read More »

Kilimo cha Binzari

tangulizi Jina la kitalaam ni Curcuma domestica na kwa kiingereza ni turmeric. Zao hili asili yake ni Mashariki ya Mbali, na linalimwa zaidi katika mkoa

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »