UGONJWA WA COLIBACILLOSIS KWA KUKU

UGONJWA WA COLIBACILLOSIS KWA KUKU

UGONJWA WA COLIBACILLOSIS KWA KUKU: Ugonjwa huu husababishwa na bakteria waitwao Escherichia coli. Bakteria hawa huingia mwilini kwa mnyama kwa njia ya chakula au mara tu mnyama anapozaliwa au kuku anapototolewa.

– Bakteria hawa huanza mashambulizi mara tu mnyama anapopata matatizo (stress) kwa vile kinga ya mwili hupungua.

WANYAMA HUSIKA:

• Ugonjwa hujitokeza hasa kwa vifaranga( kuanzia wiki 2-4), ndama, watoto wa mbuzi, kondoo, farasi mara tu baada ya kuzaliwa (Neonatal diarrhoea).

• Wanyama wakubwa huwa kama wabebaji wa vijidudu (Carriers) na kinyesi chao mara nyingi ndiyo chanzo cha ugonjwa huu.

DALILI KWA VIFARANGA:

• Kutokuwa na raha (depression)

• Kuacha kula

• Kuharisha uharisho mweupe

• Rangi ya kilemba na mashavu kupauka

• Vifo

VIFARANGA VIKIFA HUONYESHA DALILI ZIFUATAZO:

• Ini na bandama huvimba na huwa na vidoadoa vya damu (haemorrhage)

• Ukungu wa usaha kwenye ini, na vifuko vya hewa (Air sacs) kwenye mapafu

• Uchafu wa majimaji nje ya viungo vya mwilini.

DALILI KWA NDAMA, WATOTO WA MBUZI, KONDOO N.K

– Ugonjwa mkali (Acute form)

• Kuharisha mfululizo

• Kupungua maji mwilini

• Kufa ndani ya masaa 12

– Ugonjwa wa makali ya (wastani) kati (Subacute form)

• Kuharisha kwa muda mrefu – Siku kadhaa

• Kupungukiwa maji mwilini

• Kukonda

• Kufa kama tiba haikupatikana haraka

• Mnyama akifa utumbo (ndani) huwa umejaa makamasi (mucoid enteritis)

TIBA

KUREKEBISHA HALI YA MWILINI

(i) Upunguaji wa maji, madini na vitamini hurekebishwa kwa kutumia dawa za kufunga kuharisha Kaovit R na vitamini
kama vile vitalyt, Vitastress na dawa zingine kama Sodium, Glucose

PITIA
Kilimo cha Pilipili Manga

(ii) Wape wanyama wagonjwa chakula kizuri chenye protini ya kutosha

DAWA ZA KUTIBU

  • Doxycol katika maji ya kunywa

KINGA

1. Colirid – Kinga katika chakula: Dawa hii huzuia colibacillosis kwa kuua wadudu ndani ya mwili wa kuku/mnyama

2. Farmacid premix – Dawa hii huchanganywa na chakula na huzuia collibacillosis kwa kuua na kuzuia vijidudu (E.coli) katika chakula kabla ya kuliwa na kuku au mnyama husika.

– Ndama, watoto wa mbuzi n.k- Wapate maziwa ya mwanzo ya mama (colostrum) mara baada ya kuzaliwa, kama mama amekufa mtoto apatiwe ‘artificial colostrum’

– Vifaranga wapewe antibacterials ndani ya wiki moja baada ya kutotolewa.

– Usafi wa mazingira, vyombo na wahudumu.

– Wanyama wakubwa wasichanganywe na wadogo (newborns)

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Ujue Muhogo

MUHOGO ni moja ya mazao ya mizizi na lenye umuhimu katika mazao makuu ya chakula baada ya zao la mahindi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao

Read More »
Mpunga / mchele

KILIMO BORA CHA MPUNGA

Mpunga ni kati ya mazao ambayo yanalimwa sana dunian na pia ni kati ya mazao ambayo yanapendwa sana na watu kutokana na chakula chake kuwa

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »