Ujue Muhogo

MUHOGO ni moja ya mazao ya mizizi na lenye umuhimu katika mazao makuu ya chakula baada ya zao la mahindi nchini Tanzania.
Umuhimu wa zao hilo unatokana na uwezo wa kustawi katika mazingira tofauti ya hali ya hewa na rutuba ya udongo. Muhogo unastahimili ukame na hivyo kuitwa zao la kinga ya njaa hasa kunapojitokeza ukosefu wa mvua katika msimu husika.
Zao la Muhogo linatumika kwa kuandaa aina mbalimbali ya vyakula, ikiwa ni pamoja na ugali, chipsi, maandazi, chapati, mkate, keki na biskuti. Pia majani yake hutumika kama mboga maarufu kisamvu.

https://i0.wp.com/startvtz.com/wp-content/uploads/2017/01/pic_muhogo.jpg?w=1600
Aina za muhogo

Kuna makundi mawili ya muhogo ambazo ni muhogo mtamu na mchungu. Katika makundi hayo kuna aina zaidi ya 21 za mihogo zilizothibitishwa na wataalamu wa kilimo nchini. Aina hizo za mihogo hulimwa kwa kuzingatia hali ya hewa na udongo katika kanda husika.
Kwa mujibu wa rekodi za kilimo cha muhogo nchini, kuna kanda nne zinazojihusisha na kilimo hicho. Kuna Kanda ya Pwani inayojumuisha Naliendele, Kiroba, Mkumba, Kibaha na Pwani.
Kanda ya Kati inajumuisha Hombolo, Dodoma, Makutupora na Mumba, Kanda ya Ziwa na Magharibi inajumuisha Mkombozi, Kyaka, Meremeta, Nyakafulo na Fuma ambapo Kanda ya Zanzibar na Pemba inajumuisha Kizimbani, Mahanda na Machui na Kama.
Kutayarisha shamba
Muhogo hustawi zaidi kwenye udongo wa kichanga au ardhi tifutifu yenye rutuba ya wastani. Shamba litifuliwe vyema baada ya kufyeka na kung’oa visiki kabla ya msimu ni vyema matuta yaandaliwe ili kuwezesha ukuaji wa mizizi, kurahisisha uvunaji.
Kutayarisha mbegu
Mbegu zichaguliwe kutoka kwenye miche ya muhogo isiyoshambuliwa na wadudu na magonjwa kama batobato na michirizi ya kahawia. Mbegu hukatwa vipandepande kutoka kwenye muhogo uliostawi vizuri na vitumba vizuri vilivyo karibu na kuondoa sehemu ngumu ya shina na sehemu ya juu kuepuka sehemu laini.
(Sehemu ya katikati ya shina ndiyo inafaa kukata pingili) Pingili/vipande hukatwa kwa urefu wa sentimeta 25 hadi 30 wastani wa vitumba vinane.
Kupanda muhogo
Muhogo hupandwa mwanzoni wa msimu. Pamoja na muhogo kuvumilia ukame, mvua chache hupunguza mazao. Upandaji unaostahili ni kufukia sehemu kubwa ya ya pingili ardhini kwa kuilaza mshazari kidogo (nyuzi 45) ili macho yatakapotoa machipukizi yaelekee juu. Shindilia udongo kando ya pingili.
Nafasi za upandaji nazo zimegawanyika kutokana na aina ya udongo, aina ya muhogo wenyewe na kama muhogo unachanganya na mazao mengine. Nafasi za upandaji zilizopendekezwa ni mita moja kwa mita moja ikiwa unapanda mbegu ya muhogo unazaa sana na muhogo wake ni mirefu.
Unapaswa kuacha nafasi ya mita moja kwa sentimeta 90 ikiwa unatumia mbegu ya muhogo unaozaa sana na muhogo wake ni mfupi mnene. Unapaswa kuacha nafasi ya mita 1 kwa sentimeta 75 ikiwa unatumia mbegu ya muhogo unaozaa kwa wastani.
Mbolea
Kwa kuwa muhogo unastawi vizuri katika udongo usio na rutuba Tanzania haina rekodi rasmi kuhusu ushauri wa mbolea inayopaswa kutumiwa katika kilimo cha muhogo. Hata hivyo unaweza kutumia kutumia samadi au mboji ili kuuongezea udongo wa shamba uwezo wa kutunza unyevu hasa maeneo yenye udongo wa kichanga.

Palizi

Ni muhimu kufanya palizi katika kilimo cha muhogo na ni vyema palizi ifanyike mara tatu kwa msimu ili kuzuia magugu ambayo husababisha kunyang’anyana lishe muhogo. Pia palizi inasaidia kuondoa majani yanayotengeneza maficho kwa visumbufu vya mimea (wadudu na magonjwa).
Kurudisha udongo kwenye mashina wakati wa palizi huongeza mazao.Visumbufu vya muhogo Ingawa muhogo unahimili ukame unaweza kuathiriwa na visumbufu yaani wadudu mbalimbali ikiwa ni Cassava whitefly wadudu weupe wanaoshambulia muhogo, cassava green mites (CGM), wadudu ambao hushambulia majani mapya ya muhogo hasa sehemu za chini na Scales yaani wadudu wanaojishika kwenye shina na kufyonza maji kutoka kwenye mti wa muhogo.
Visumbufu vingine ni cassava mealbugs yaani wadudu wanaoshambulia kwenye ncha za mashina/matawi kwenye majani machanga. Athari zake ni kwamba majani yanadumaa na kujikusanya pamoja, hivyo basi kupunguza ukuaji wa mmea kwa ujumla. Vile vile urefu kati ya pingili na pingili huwa fupi sana. Pia visumbufu kama mburumundu, nzige na vidugamba huathiri mihogo.
Visumbufu karibu vyote vilivyotajwa hapo juu vinashambulia muhogo kwa kufyonza majani na kuleta madhara kwa namna tofauti na kusababisha uzalishaji duni wa muhogo Ili kuvidhibiti visumbufu hivyo unapaswa kuwasiliana na mtaalamu wa kilimo aliyepo karibu nawe kwa ushauri wa kina.
Magonjwa
Yapo magonjwa mengi ya muhogo lakini ugonjwa wa Batobato ndiyo unaosumbua sana wakulima hapa Tanzania. Ugonjwa wa batobato husababisha majani yakunjamane na kuwa ya njano na mwisho hupuputika na kufanya mmea kudumaa na kushindwa au kutowa mazao hafifu na yasikuwa na ubora, ugonjwa huu huenezwa na inzi mweupe (cassava whitefly).
Kuzuia
Unashauriwa kutumia mbegu za muhogo zinazokinzana na ugonjwa wa batobato (waone wataalamu kwa ushauri). Kuvuna Muhogo huanza kukomaa kuanzia mwezi wa nane hadi 12 tangu kupandwa shambani hii kulingana na aina ya mbegu. Uvunaji hufanyika kwa kuchimba na kung’oa shina lote au kutoa baadhi ya muhogo na kuacha shina liendelee pale shambani.

KILIMO BORA CHA MIHOGO
Zao la muhogo ni muhimu sana kwa Tanzania zaidi kwa wakulima wadogo wenye kipato cha chini. Wakulima wengi huchanganya zao la muhogo na mazao mengine kama vile kunde, mbaazi, njugumawe, n.k. Umuhimu wa zao hili ni kutupatia cahakula na wakati mwingine kwa biashara. Kwa kanda ya kusini muhogo ni chakula kikuu ambacho kinachukua asilimia 75 ya chakula kwa maeneo yote ya mikoa ya pwani
Muhogo hustawi vizuri katika maeneo yaliyopo kwenye maeneo ya mita 0 – 1500 kutoka usawa wa bahari. Vile vile muhogo hustawi vizuri kwenye maeneo yanayopata mvua ya wastani wa mm 750 – mm1200 kwa mwaka. Muhogo hustawi vizuri kwenye ardhi ya kichanga. Vili vile zao la muhogo ni maarufu sana kwa uvumilivu wa hali ya ukame.

PITIA
Kilimo cha Kabichi

TEKNOLOJIA ZILIZOPO

i. Mbegu bora za muhogo
Mpaka sasa hivi kuna aina mbili za mbegu bora ambazo zimathibitishwa kwa wakulima. Mbegu hizi huvumilia magonjwa, (batobato na matekenya), pia huzaa sana ukilinganisha na mbegu za kienyeji.
• Naliendele
Huzaa tani 19 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.
• Kiroba
Huzaa tani 25 – 30 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.
ii. Mbinu bora za kilimo cha muhogo
• Uandaaji wa shamba
Shamba liandaliwe kabla ya msimu wa kuanza. Uandaaji wa shamba bora hufuata hatua zifuatazo:
– Kufyeka shamba
– Kung’a na kuchoma visiki
– Kulima na kutengeneza matuta
• Uchaguzi wa mbegu bora za kupanda
Mbegu zinatakiwa zisiwe na magojwa yeyote, pia chagua mashina ambayo yamelomaa vizuri.
• Upanadaji
Kuna njia tatu za upandaji wa muhogo:
– Kulaza ardhini (Horizontal)
– Kusimamisha wima (Vertcal)
– Kuinamisha ( Inclined/Slunted)
Urefu wa kipande cha shina cha kupanda:
Inashauriwa urefu uwe sm 30; lakini urefu wa kipande cha kupanda unategemea sana idadi ya macho yaliyopo kwenye hicho kipande, inashauriwa kipande kiwe na macho (4 – 6).
Nafasi ya kupanda:
Kwa upandaji wa shamba muhogo tupu, shina hadi shina ni mita 1 na mstari hadi mstari ni mita 1.Kwa shamba la mchanganyiko na mazao mengine, inategemeana na zao linalochanganywa; mstari hadi mstari ni mita 2 – mita 4 na shina hadi shina ni mita 1.
• Palizi:
– Palizi ya kwanza ifanyike mapema (mwezi 1) baada ya kupanda ili kuepukana na magugu yanayochipua haraka baada ya mvua kunyesha. Ndani ya miezi mine ya mwanzo mihogo haitakiwi kuwa na magugu ili kuepuka ushindni wa mahitaji muhimu (mwanga, mbolea, maji, n.k) kati ya muhugo na magugu.
– Palizi hufanyika kwa kutumi jebe la mkono au dawa ya kuuwa magugu.
– Wakati mwingine udhibiti wa magugu kufanyika kwa kutumia majani kwa kutandazwa juu ya udongo.
– Plaizi hufanyika mara 2 – 3 hadi muhugo kukomaa.
• Uvunaji:
Mihogo inaweza kuanza kuvunwa baada ya miezi 9 – 12 tangu kupandwa. Inashauriwa kuvuna katika katika kipindi cha jua; kwani wakati wa mvua kiwango cha wanga kwenye muhogo hupungua.
• Usindikaji bora
Usindikaji bora wa muhogo unafanyika kwa sababu kuu mbili:
– Kurahisisha/kuharakisha ukaushaji
– Kuondoa sumu (cyanide) ilyoko kwenye baadhi ya aina za mihogo
– Kuongeza ubora wa unga utokanao muhogo wenyewe.
Njia bora za usindikaji
– Kwa kutumia mashine aina ya Grater
Hii hutoa chembechembe laini za muhogo, ambazo baadae hukamuliwa kwa kutumia kifaa kingine kiitwacho “presser” ili kuondo sumu iliyoko kwenye muhogo. Mashine hii hutumika hususani kwa muhogo mchungu.
– Kwa kutumia mashine aina ya chipper
– Mashine hii hutoa vipande vidogo vidogo (chips). Mashine hii hutumika hasa hasa kwa ajili ya mihogo mitamu/baridi.
Matumizi ya Muhogo
– Muhogo unaweza kupikwa wenyewe kama chakula au kutengeneza unga
– Unga wa muhogo unaweza kutengeneza vitu vyotekama vinavyotengenezwa na unga wa ngano kama vile biskuti, chapatti, maandazi, chichili, keki n.k.
– Pia muhogo huweza kutumika viwandani kutengeneza bidhaa nyingine kama vile wanga.
iii MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
• Magonjwa
Kuna magonjwa mawili ambayo ni muhimu sana na yanapunguza uzalishaji wa zao la muhogo.
a) Ugonjwa wa Matekenya au Ugonjwa wa michirizi ya kahawia
katika muhogo
Ugonjwa huu ni maarufu kwenye sehemu zenye miinuko iliyo na urefu chini ya mita 300 na unapatikana kidogo sana kwenye miinuko ya mita 500 na kuendelea ambako uenezaji wake wa kawaida hautokei kabisa.
Visababishi:
Matokeo ya uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba ugonjwa huu ulienezwa na mdudu mweuupe au inzi mweupe (whitefly) mwenye mabawa madogo.
Dalili za Ugonjwa
Sehemui zote za muhogo zinaweza kuonyesha dalili za uambukizo wa ugonjwa huu lakini ni vipengele gani vya ugonjwa na ni kwa kiwango gani hutegemea hali ya mzingira, hatua ya kukua kwa mmea kwa kulinganisha.
– Kwenye majani
Dalili ya kwanza: Chlorosis rangi ya njani hutokea kwanza pembezoni mwa vena ndogo baadae huathtiri vena ndogo zaidi na inaweza kuwa doa (chlorosis) la rangi ya njano.
Dalili ya pili: Rangi ya njano ambayo haihusishwi vizuri na vena isipokuwa katika mbaka ya mviringo kati ya vena kuu kwenye hatua za mwisho za ugonjwa sehemu kubwa ya lamin inaweza isiathirike, majni yenye ugonjwa hubaki yameshikilia kwenye mmea kwa muda wa wiki kadhaa.
– Kwenye shina
Huonekana kwenye tisu ya shina changa la kijani, jeraha la zambarau au kahawia linweza kuoneakan nje na kuingia ndani hadi kwenye gamba baaada ya kubandua gome la nje. Pia jeraha la nekrotiki kwenye kovu la shina hutokea baada ya majni kudondoka kutokana na umri wa mmea. Tawi/shina hufa kuanzia kwenye nch kuelekea chini na kusababisha kufa kwa mmea wote.
– Kwenye mizizi
Kwa kawaida hutokea baada ya dalili za majani na wakati wa kipindi kati ya uambukizo na kufa, amabpo kifo cha mizizi hutokea kuanzia miezi 5 toka kupandwa. Dalili za mizizi zinabadilika nje ya mizizi na zinaweza kuwa kama kizuizimwanga au shimo au kufa kwenye gome.
Tishu inayo zunguka mshins ina doa la rangi ya kahawia au nyeusi. Wakati mwingine mizizi huonekana kuwa yenye afya kwa nje bila kuwa na matatizo yaliyowazi au bila kupungua ukubwa, lakini ikikatwa huonekana kufainakufa au rangi ya njano.
Uambukizaji na ueneaji
Ugonjwa wa CBSD unaambukizwa kwa njia ya vipandikizi vinavyotokea kwenye mimea iliyoathiriwa vinavyosababisha mmea kuonesha kwenye majani dalili za ugonjwa.
Kwa kuwa muhogo kwa kawaida huzalishwa kwa njia ya vipandikizi ugonjwa huu huingizwa kwenye sehemu mpya zilizopandwa kwa kutumia vipandikizi vilivyoambukizwa.
Kwa aina zinazovumilia sana kwenye hali za mabondeni, dalili mbaya sana hutokea wakati ugonjwa ukigundulika katika hatua za mwanzo.
Uchunguzi umeonesha kwamba Bemisia afer ni mdudu/kisababishi ambacho ndicho kinachohusiana na maendeleo ya hivi karibuni kuhusu uhamishaji wa visababishi kama “ipomovirus”. Mara nyingine inaonesha nzi weupe (White flies) na kutokana na hali hiyo bado uchunguzi unaendelea zaidi.
Udhibiti/Kuzuia
Njia ya msingi ya kuzuia/kudhibiti ugonjwa wa CBSD ni kuchagua mbegu kutoka kwenye mimea isiyo na dalili ya ugonjwa.
Ubora wa mashina unahitaji kutunzwa kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza ile iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua.
Hakikisha kuwa unapanda mbegu bora za mhogo ambazo zinastahimili uambukizo wa magonjwa.
Hakikisha kuwa wakati wa uvunaji uonapo hali ya kuoza kwa mizizi ya mhogo ichome moto ili kutokomeza ugonjwa huo.
Kuelewa dalili za ugonjwa wa CBSD kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya kutokomeza ugonjwa huu.
Hakikisha kuwa unaendelea kutunza mbegu bora zinazoonekana kuvumilia magonjwa sana.
Hakikisha kuwa shamba la mhogo linakuwa safi kwa ajili ya kupunguza visababishi vya ugonjwa wa CBSD
b) Ugonjwa wa batobato au ukoma wa majani
Ni ugonjwa ambao ulienezwa kwamara ya kwanza hapa Tanzani mwaka 1894, na baadae uliripotiwa katika nchi nyingine nyingi za Afrika Mashriki, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati na sasa unafahamika kuwa upo maeneo yote yanayolimwa muhogo Afrika.
Katika viwango vya kuwepo kwa ugonjwa wa CMD na katika uwingi wa hasara zinazopatikana kutokana na CMD ni kati ya 15% – 20%. Hii ni sawa na tani milioni 15 – 18 zikilinganishwa na makadirio ya shirika la kilimo na chakula duniani ya tani milioni 85 ya mwaka 1997.
Visababishi
Tangu ugonjwa wa CMD ulipoenezwa kwa mara ya kwanza, visababishi vilichukuliwa kuwa ni virusi kwa sababu ya kukosekana kisababishi kingine. Kwa hiyo kutokana na kuwa mtazamo huu unalingana na matokeo ya uchunguzi wa awali inaonesha kwamba ugonjwa huu huenezwa na nzi mweupe (white fly).
Pia uchunguzi wa mara kwa mara umesababisha utambuzi wa virusi vya aina mbalimbali na tofauti kama ifuatavyo:
• Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Africa cassava mosaic virus
• Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Afrika mashariki (East Africa cassava mosaic virus)
• Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya India (Indian cassava mosaic virus)
Dalili za ugonjwa wa batobato (Cassava Mosaic Disease-CMD)
Dalili hutokea kwenye jani lenye uwaraza wa michirizi ambazo huathiri
Sehemu zisizokunjamana za kutolea hewa na hufahamika katika hatua za
Awali za ukuaji wa jani.
Sehemu za kloritiki hushindwa kutanuka hadi mwisho, hivyo mvutano unaji-
tokeza kutokana na ukuaji usiolingana na jani au majani madogo yaliyoharibika.
Majani yaliyoathirika sana hupungua ukubwa wa umbo, na hujikunja na kujitenga kwa
Sehemu zenye rangi ya njano na zenye rangi ya kawaida ya kijani.
Mmea hudumaa na majani machanga hupatwa na uvimbe.
Kloritiki ya jani inaweza kuwa ya rangi ya manjano nyepesi au rangi inayokaribia nyeupe
yenye kijani kidogo au kupauka kuliko ilivyo kawaida.
Uambukizaji na uenezaji
Ukoma wa mhogo huambukizwa kwenye vipandikizi vya shina ambavyo kwa kawaida
hutumika kuzalishia mmea.
Pia huenezwa na inzi mweupe (white fly) aitwae Bemisia tabaci G. Aina mbili za inzi au
Mbu hao Bemisia (Preisner Hhosny na Aleorodius disperses R) pia huambukiza mihogo
katika nchi za Afrika na India
Usambazaji wa vipandikizi unaweza kusababisha kuenea kwa ugonjwa wa CMD katika
Maeneo mapya.
UHIBITI NA KUZUIA
-Hatua ya msingi ya kuzuia ugonjwa wa CMD ni kwa kuchagua vipandikizi kutoka kwa
Mmea ambao hauna uambukizo wowote.
-Ubora wa mashina unahitajika kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza kwa kung’oa ile
Mihogo iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua
-Hakikisha kuwa wakati wa kuvuna mihogo kwa ile iliyoathirika na ugonjwa wa CMD
inaangamizwa kwa kuchomwa moto.
-Hakikisha kuwa unatunza shamba na kuwa safi ili kupunguza wadudu waenezao CMD.
-Hakikisha una elimu ya kutosha juu ya dalili za ugonjwa wa CMD>
• WADUDU NA WANYAMA WAHARIBIFU
– Cassava Mealy Bug (CMB)
Wadudu hawa hushambulia kwenye ncha za mashina/matawi kwenye majani machanga. Athari zake ni kwamba majani ynadumaa na kujikusanya pamoja, hivyo basi kupunguza ukuaji wa mmea kwa ujumla. Vile vile urefu kati ya pingili na pingili huwa fupi sana.
– Cassava Green Mites (CGM)
Wadudu hawa hushambulia majani mapya sehemu za chini. Madhara yake sio makubwa.
– White Scales
Hawa ni weupe na hujishika kwenye shina na kufyonza maji kutoka kwenye mti wa muhogo. Vili vile wadudu hawa madhara yake sio muhimu.
– Mchwa
Hawa hutafuna/hula mashina ya muhogo hasa wakati wa jua kali/kiangazi.
– Wanyama waharibifu
Hawa hushambulia muhogo ukiwa shambani kwa kuula, kama vile nguruwe, panya, wezi, n.k
Udhibiti/Kuzuia
Kwa upande wa wadudu wanweza kudhibitiwa kwa njia zifuatazo:
Kutumia dawa za kuulia wadudu
Kutumia wadudu marafiki wa wakulima
Kwa upande wa wanyama ni kuweka walinzi.

PITIA
KILIMO BORA CHA KAROTI

KUTAYARISHA SHAMBA

Muhogo hustawi zaidi kwenye udongo wa kichanga au ardhi tifutifu yenye rutuba ya wastani.

Shamba litifuliwe vyema baada ya kufyeka na kung’oa visiki kabla ya msimu ni vyema matuta yaandaliwe ili kuwezesha ukuaji wa mizizi, kurahisisha uvunaji.

KUANDAA MBEGU
Mbegu zichaguliwe kutoka kwenye miche ya muhogo isiyoshambuliwa na wadudu na magonjwa kama batobato na michirizi ya kahawia. Mbegu hukatwa vipandepande kutoka kwenye muhogo uliostawi vizuri na vitumba vizuri vilivyo karibu na kuondoa sehemu ngumu ya shina na sehemu ya juu kuepuka sehemu laini.
(Sehemu ya katikati ya shina ndiyo inafaa kukata pingili) Pingili/vipande hukatwa kwa urefu wa sentimeta 25 hadi 30 wastani wa vitumba vinane.

KUPANDA MHOGO
Muhogo hupandwa mwanzoni wa msimu. Pamoja na muhogo kuvumilia ukame, mvua chache hupunguza mazao. Upandaji unaostahili ni kufukia sehemu kubwa ya ya pingili ardhini kwa kuilaza mshazari kidogo (nyuzi 45) ili macho yatakapotoa machipukizi yaelekee juu. Shindilia udongo kando ya pingili.
Nafasi za upandaji nazo zimegawanyika kutokana na aina ya udongo, aina ya muhogo wenyewe na kama muhogo unachanganya na mazao mengine.

Nafasi za upandaji zilizopendekezwa ni mita moja kwa mita moja ikiwa unapanda mbegu ya muhogo unazaa sana na muhogo wake ni mirefu.
Unapaswa kuacha nafasi ya mita moja kwa sentimeta 90 ikiwa unatumia mbegu ya muhogo unaozaa sana na muhogo wake ni mfupi mnene. Unapaswa kuacha nafasi ya mita 1 kwa sentimeta 75 ikiwa unatumia mbegu ya muhogo unaozaa kwa wastani.

MBOLEA
Kwa kuwa muhogo unastawi vizuri katika udongo usio na rutuba Tanzania haina rekodi rasmi kuhusu ushauri wa mbolea inayopaswa kutumiwa katika kilimo cha muhogo. Hata hivyo unaweza kutumia kutumia samadi au mboji ili kuuongezea udongo wa shamba uwezo wa kutunza unyevu hasa maeneo yenye udongo wa kichanga.

PITIA
KANUNI BORA ZA KILIMO CHA MACHUNGWA

PALIZI
Ni muhimu kufanya palizi katika kilimo cha muhogo na ni vyema palizi ifanyike mara tatu kwa msimu ili kuzuia magugu ambayo husababisha kunyang’anyana lishe muhogo. Pia palizi inasaidia kuondoa majani yanayotengeneza maficho kwa visumbufu vya mimea (wadudu na magonjwa).
Kurudisha udongo kwenye mashina wakati wa palizi huongeza mazao.Visumbufu vya muhogo Ingawa muhogo unahimili ukame unaweza kuathiriwa na visumbufu yaani wadudu mbalimbali ikiwa ni Cassava whitefly wadudu weupe wanaoshambulia muhogo, cassava green mites (CGM), wadudu ambao hushambulia majani mapya ya muhogo hasa sehemu za chini na Scales yaani wadudu wanaojishika kwenye shina na kufyonza maji kutoka kwenye mti wa muhogo.
Visumbufu vingine ni cassava mealbugs yaani wadudu wanaoshambulia kwenye ncha za mashina/matawi kwenye majani machanga. Athari zake ni kwamba majani yanadumaa na kujikusanya pamoja, hivyo basi kupunguza ukuaji wa mmea kwa ujumla. Vile vile urefu kati ya pingili na pingili huwa fupi sana. Pia visumbufu kama mburumundu, nzige na vidugamba huathiri mihogo.
Visumbufu karibu vyote vilivyotajwa hapo juu vinashambulia muhogo kwa kufyonza majani na kuleta madhara kwa namna tofauti na kusababisha uzalishaji duni wa muhogo Ili kuvidhibiti visumbufu hivyo unapaswa kuwasiliana na mtaalamu wa kilimo aliyepo karibu nawe kwa ushauri wa kina.

MAGONJWA
Yapo magonjwa mengi ya muhogo lakini ugonjwa wa Batobato ndiyo unaosumbua sana wakulima hapa Tanzania. Ugonjwa wa batobato husababisha majani yakunjamane na kuwa ya njano na mwisho hupuputika na kufanya mmea kudumaa na kushindwa au kutowa mazao hafifu na yasikuwa na ubora, ugonjwa huu huenezwa na inzi mweupe (cassava whitefly).
Kuzuia
Unashauriwa kutumia mbegu za muhogo zinazokinzana na ugonjwa wa batobato (waone wataalamu kwa ushauri). Kuvuna Muhogo huanza kukomaa kuanzia mwezi wa nane hadi 12 tangu kupandwa shambani hii kulingana na aina ya mbegu. Uvunaji hufanyika kwa kuchimba na kung’oa shina lote au kutoa baadhi ya muhogo na kuacha shina liendelee pale shambani.

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »