Umwagiliaji wa Matone

Umwagiliaji wa matone ni mfumo wa kisasa kwa umwagiliaji wa mimea na hasa mazao. Maji hupelekwa polepole kwa mabomba au mipira yenye matundu madogo moja kwa moja hadi mguu wa kila mmea, karibu na mizizi yake. Mfumo huu unapunguza sana matumizi ya maji na pia shida nyingine mbalimbali.[1][2]

Vyanzo vya mfumo huu vinajulikana kutoka China ya Kale ambako wakulima walizika sufuria za kauri katika ardhi karibu na miti na kuizijaza maji, Maji yalipita kwenye kuta za vyombo na kuingia udongo karibu na mizizi polepole. Wajerumani walitumia mabomba ya udongo wa ufinyanzi uliochumwa ndani ya ardhi kwa umwagiliaji kuanzia karne ya 19. Baada vita kuu ya pili ya dunia mtu wa Australia alianza kutumia mabomba ya plastiki yenye matundu.

Ilionekana ya kwamba mbinu huu ni rahisi lakini una hasara kama mpira ni ndefu. Matundu karibu na chanzo cha maji hutoa maji zaidi kuliko matundu ya mbali. Pia kama shinikizo katika mpira ni juu kidogo maji hayatokei kwa umbo la matone mbali kwa nguvu mno kama mwendo mfululizo. Mfumo huu uliboreshwa nchini Israeli na Simcha Bass aliyeongeza nozeli za kutonesha maji (ing. dripper au emitter). [3]

Katika maeneo ya joto kubwa mfumo wote hupelekwa chini ya uso wa ardhi kwa kupunguza tena upotevu kutokana na usimbishaji wa maji hewani.

Faida za umwagiliaji wa matoneEdit

Faida za umwagiliaji wa matone ni kama zifuatazo:
◾Matumizi ya maji ni kidogo
◾Mbolea wa chumvi unaweza kuongezwa katika maji na kufikishwa karibu na mizizi pekee, hivyo matumizi yake yapungua pia
◾Maji yapelekwa pale amboka mimea inayahitaji, siyo pale ambako haihitajiki
◾Magugu yanapungua kwa sababu hayamwagiliwi (isipokuwa sehemu iliyo karibu sana na mazao)
◾Hatari ya magonjwa wa fungus inapungua kwa sababu majani yanabaki makavu
◾mfumo unahitaji shinikizo kidogo tu na hii inapunguza gharama za nishati (diseli, umeme) kwa ajili ya pampu
◾hata pampu ni ndogo hivyo rahisi zaidi
◾Mmomonyoko wa ardhi shambani unapungua sana
◾Hatari ya kuongezeka kwa chumvi ardhini inapungua sana

Jiunge Nasi Telegram

Usipitwe na Nyaraka mpya kila zikiwekwa kwenye Tovuti yetu na weza kujifunza kwa kina ukitumia simu. Jiunge sasa hapa.

Kilimo cha Kunde

KUNDE – COWPEAS (vigna unguiculata) UTANGULIZI Kunde ni zao ambalo linaweza kulimwa kwa ajili ya chakula na bishara ni zoa lenye kiasi kukubwa cha protini

Read More »

UFAHAMU MFUMO WA KILIMO SHADIDI

Mfumo wa kilimo shadidi cha mpunga (MKiShaMpunga) unaojulikana kwa Kimombo kama ‘Sytem of Rice Intensification’ au ‘SRI’ kwa ufupi unajumuisha mbinu  vumbuzi za kilimo ambazo

Read More »